Wednesday, February 5, 2014

BIOGRAPHY : TREY SONGZ

   Tremaine Aldon Neverson, kwa jina la Kikazi anajulikana kama Trey Songz ni Rapper, songwriter, mwimbaji, muigizaji na pia produza .
Album yake ya kwanza ilikuwa imetoka mwaka 2005 iitwayo "i gotta make it " ikafuatiwa na ya pili mwaka 2007 iitwayo "trey day", mwaka 2009 trey aliamua kutoa album yake ya tatu iitwayo "Ready".  Album yake ya "Passion, Pain & pressure" ambayo ilikuwa ya nne ilitoka Sept,14-2010 na ikafuatiwa na album yake ya tano iitwayo "Chapter V" ambayo aliitoa Aug,12-2012 .











EARLY LIFE :

 
      Tremaine Aldon Neverson a.k.a Trey Songz alizaliwa November ,28-1984 kwenye ki-mji kidogo kusini mwa Richmond huko Petersburg ,virginia. Mama yake ,April Tucker alikuwa anamiaka 17 wakati Trey alivyokuwa amezaliwa. Wakati Trey ana umri wa miaka 7 ,mama yake aliolewa na mwanajeshi kwahiyo Trey alilelewa katika maisha ya kuhama sehemu tofauti wakati kila sehemu ambayo Baba yake wa kambo alipokuwa anahamishwa kikazi. 
   Trey alijigundua uwezo wake wa kuimba na kutunga mashairi wakati familia yake imerudi Petersburg ambapo alikuwa ana umri wa miaka 14 . Trey alianza kupafom huku akipewasupport kubwa na ndugu na marafiki zake. Produza Troy Taylor aligundua uwezo wa Trey 2000 kwenye moja ya Talent Show na kukubaliana kwamba amalize shule(high school) ndipo waanze kazi ya Muziki pamoja. Trey wakati amemaliza High school akahamia New Jersey ilikuanza kazi yake ya Muziki.

Endelea KUFAHAMU mengi HAPA CHINI...



MUSIC CARRIER: 

   Mwaka 2013 ,Trey alisign dili ya muziki katika studio iitwayo Atrantic Records na kupokea kitita cha fedha $100,000 . Baada ya miaka miwili ndio alipoachia  Album yake ya kwanza I gotta make it ,hii album haikufanya vizuri zaidi kwahiyo akashika nafasi ya 20 kwenye Billboard Album charts na kuuza kopi 395,000 ,lakini mwaka 2007 alipanda zaidi baada ya kutoa Album yake ya pili, Trey day iliyokuwa na kibao cha Can't help but wait, na hicho kibao kushika nafasi 11 kwenye Billboard Charts. TRey aliendelea zaidi kupanda katika Album yake ya tatu ,Ready ambayo ilishika nafasi ya 3 katika Billboard Album charts na kukubalika kimuziki zaidi katika Radio tofauti na pia kupata tuzo ya BET-2010 ya BEST  MALE R&B ARTIST.

Tazama Picha za TREY HAPA CHINI...

MAMA YAKE APRIL TUCKER



CLASSIC PICZ : 






TREY'S SMILE :





TREYZ BODY:






Source : www.biography.com
               www.wikipedia.com
               www.google.com